Jina
la Kanisa:T.A.G - Songea Revival
Church
Kauli Mbiu: Tumeitwa
Kumtumikia Mungu Kwa Viwango Vyenye Ubora Wa Hali Ya Juu
Kauli Ya Umisheni: Kumwandaa
Kila Mwamini Hadi Awe Amejazwa Na Nguvu Za Roho Mtakatifu Ili Awe Chombo Cha Kuwaleta Kwa
Yesu Waliopotea Dhambini.
Maono Ya Kanisa: Kuwajenga Waliofikiwa Ili Waweze Kuwafikia
Wengine.
Historia Ya Kanisa:


Kanisa la TAG Songea Revival lilifanikiwa kununua kiwanja
cha kanisa mwaka 2010 mwezi Januari, na ujenzi ulianzamwezi Juni tarehe ya
mosi, 2010. Mkono wa Bwana ulikuwa juu ya uongozi wa Kanisa hili kiasi kwamba
hadi kufikia siku ya ibada ya kuweka Jiwe la Msingi jumla ya kiasi cha Tsh. 75,200,000/= zilipatikana na kutumika kwa
ujenzi wa jengo lake la kuabudia.
Ibada ya kuweka Jiwe la Msingi ilifanywa na Askofu Mkuu
wa Tanzania Assemblies of God, Rev. Dr. Barnabas Weston Mtokambali April 27,
2011, miezi kumi tangu ujenzi ulipoanza.
Hadi wakati huo wa kuweka jiwe la msingi, Songea Revival lilikuwa
na jumla ya washirika mia moja na arobaini; (140), yaani watu wazima 80 na
watoto 60, ambao kwa umoja wetu Bwana alitupatia neema ya kuanzisha ujenzi wa
jengo la kuabudia. Kiasi hiuki cha fedha; yaani 75,200,000/= kimchanganuo,
Tshs.21,000,000/= zilipatikana kama mkopo. Tshs. 9,700,000/= zilitoka katika mfuko wa sadaka
na mafungu ya kumi ya wana–Songea Revival. Tshs.19,100,000/= hizo zilikuwa changizo iliyofanywa na Wana
Songea Revival. Tshs 3,900,000/= ilikuwa michango ya marafiki wa TAG–Songea
Revival. Na Tshs. 21,500,000/= ulikuwa
mchango wa Mch. Fussi kama Injinia wa Jengo.
WASHIRIKA
|
MAKUSANYO YA UJENZI WA KANISA
|
||||
Wkubwa
|
Wtoto
|
Mkopo (Tzs)
|
Kikumi (Tzs)
|
Changizo (Tzs)
|
Misaada (Tzs)
|
80
|
60
|
21,000,000/=
|
21,500,000/=
|
19,100,000/=
|
3,900,000/=
|
Muundo Wa Jengo La TAG-Songea Revival
Jengo hili la Kanisa limejengwa katika kiwanja cha ukubwa
wa mita za mraba 780 yaani mita 26 kwa mita 30. Kiwanja hiki kinatambuliwa kama
Kiwanja No. 315 Kitalu B-B MAHENGE, ambacho kina jina la TANZANIA ASSEMBLIES OF GOD-Songea Revival.
Kiwanja hiki kina Ukumbi wa jengo lenye ukubwa wa mita 13
x 27. Vyumba 7, yaani vi-5 ni ofisi za kanisa, kimoja Jiko, viwili stoo. Kila
idara ina Ofisi yake. Chumba kimoja kilicho juu ghorofani kimebuniwa kuwa Cha
Kulala Wageni; nacho ni Self-Contained. Jengo lina chemba 6 za
Vyoo vya kisasa. Chemba nne kwa matumizi ya Public na mbili kwa
matumizi ya Private. Ndani ya jengo hili pia kuna sehemu maalum ya
kubatizia waongofu wapya; inajulikana kama “Yordani”. Aidha juu kuna sehemu
maalumu kwa ajili ya Projetor.

No comments:
Post a Comment