Karibu Songea Revival Church

Karibu  Songea Revival Church

Huduma za Songea Revival Church

Huduma za Songea Revival Church

Huduma



HUDUMA ZINAZOTOLEWA:
Uongozi wa Idara Kanisa la Songea Revival una wajibu wa kuwalea vijana na kuwapa fursa ya kutumika katika ujenzi wa kazi ya Mungu.

IDARA YA CA’s
Mkurugenzi: Jeremia Kayanda |+25576464206 |
Kama maandiko matakatifu yasemavyo katika 2Korintho 5:20 “… tu wajumbe kwa ajili ya Kristo, kana kwamba Mungu anasihi kwa vinywa vyetu; twawaomba ninyi kwa ajili ya Kristo mpatanishwe na Mungu.
Kanisa la TAG Songea Revival lina nafasi kwa ajili ya vijana wakristo wanaopenda kumtumikia Mungu. Chama cha vijana hawa wana fursa ya kukusanyika pamoja na kuwa na wakati wa mashauriano yanayowaongoza kuainisha majukumu yao na kisha kuyafanyia uamuzi wa nini watapenda kufanya katika kutimiza wajibu wao kwa BWANA.
Ni jambo la fahari kwa vijana wa kanisa la Songea Revival ya kwamba yanawenda sambamba na mwongozo wa idara ya CA’s Taifa. Wao kama vijana wa kanisa la mahali pamoja wanatambua kwamba maisha sio suala la kula na kunywa pekee bali furaha katika Roho Mtakatifu ambayo kwa hakika hiyo hutokana na  kuifanya kazi ya Bwana Yesu. Kwa sababu hiyo hasa idara ya CA’s katika kanisa la mahali pamoja wana program nyinginezo kama ifuatavyo:-
1.     Kuna Programu ya Uinjilisti; (CA’s Out Reach Movement)
Hiki ni kikundi cha kufanya mikutano ya injili katika sehemu mbalimbali za mjini na hata katika vijiji vilivyo ndani na nje ya Wilaya ya Songea. Kupitia mikutano hiyo CA’s wanaimarisha makanisa machanga na kuanzisha makanisa mengine mapya ya vijijini na mijini.
Kwa upande mwingine kanisa la SRC lina idara ya CA’s Huduma Ya Mashuleni. Idara hiyo hushughulika zaidi na kutoa huduma ya injili mashuleni na vyuoni kwa kila siku ya ijumaa mchana kwa mujibu wa ratiba ya vipindi vya duini mashuleni.
Kitengo hiki cha huduma ya Injili mashuleni kinajumuisha shughuli za kuwafikia wanafunzi wa shule za msingi, shule za sekondari, vyuo na vyuo vikuu vilivyopo hapa Songea. Kitengo hiki chini ya mchungaji kiongozi wa SRC huandaa masomo ya kibiblia nay a kiumisheni na kuyafundisha katika madarasa yao au hata katika eneo la hapa kanisani. Nia ni kuwapandia vijana uelewa sahihi wa kibiblia kuhusu imani ya kweli na hivyo kuwa imara katika vipindi hivi vya mafundisho potofu yaliyozagaa katika nchi yetu. Ni imani yetu kuwa masomo kama hayo ni hakika yatawaandaa watumishi walei ndani na nje ya kanisa la T.A.G.

2.     Kuna Programu ya “Kikombe cha Imanueli”; (Immanuel Cup)
Kikombe cha Imanuel au Immanuel Cup, ni daraja baina ya kanisa la Songea Revival na vijana walioko mashuleni. Ni kitengo kinachohusika na michezo mashuleni. Kazi yake kubwa ni kuratibu timu za shule ili:-
a.      Kukuza vipaji vya michezo miongoni mwa wanafunzi mashuleni.
b.     Kuwajenga wanafunzi katika hali ya ukakamavu na moyo wa kujituma
c.      Kuwafanya wanafunzi kuwa na wakati wa kujengwa katika maadili mema.
d.     Kuwapa fursa wanafunzi ya kusikiliza maneno ya Mungu.
e.      Kuwajengea wanafunzi maziungira ya kuwa wabunifu katika kutatua shida zao za kisaikolojia, kijinsia na hata za kibayolojia.

3.  Kuna kuna Programu ya Usiku wa Wanafunzi (Campus Night Moments)
Katika kitabu cha Mithali 4:13-15 Neno la Mungu linasema (mstari wa 13) Mkamate sana Elimu wala Usimwache aende zake, Mshike maana yeye nui uzima wako. (mstari. 14) Usiingie katika njia ya waovu, wala usitembee katika njia ya wabaya. (mstari wa 15) Jiepushe wala usipite karibu nayo. Igeukie mbali ukaende zako.
Neno la Mungu linawaasa vijana kupita mbali na njia za uovu. Na kwa kujua kwamba hakuna kitu kinachoweza kumsaidia kijana kapambana na vishawishi vya ujana ila ni ile nguvu itokanayo na neema ya Mungu ambayo kwa kupitia neno la Mungu wanaweza kushinda nguvu za mabadiliko katika kipindi cha ujana.
 Kama vijana ;
  • Tunawasaidia vijana waliopo ndani ya kanisa letu lakini vile vile wale waliopo nje na kanisa letu, ili wote kama Sehemu ya vijana wa taifa letu wanapata fursa za kusaidiwa kimaadili, na kiroho.
  • Kwa njia ya semina mbalimbali tunawajengea uwezo vijana ili waweze kuwa na msukumo wa kiujasiria-mali ili kujikwamua kiuchumi ili kuondokana na umasikini wa kipato.
  • Kupitia mazungumzo ya kijamii katika michezo, riadha, vichekesho, maigizo, ngoma, vijana wanaweza kuwahudumia vijana wengine kwa njia iliyo nyepesi.
Idara hii ya vijana ina ofisi iliyosheheni miudombinu ya kisasa kama vile, kompyuta na printa zake, meza, kabati za kuhifadhia mafaili mbalimbali. Aidha idara hii ina  uongozi makini na thabiti. Kama unataka kujifunza uongozi kwa vitendo na kwa nadharia au mambo mengine ya maisha unakaribishwa.  Rangi au dini yako kwetu sio kikwazo.
Kitu Ya Kufanyika Katika Programu Ya Usiku Wa Wanafunzi (Campus Night)
Wanafunzi hukusanyika pamoja mara moja kwa mwaka kwa ajili ya kuwa na usiku wa ushirika wa pamoja, ili kupata burudiko, mapumziko, mazungumzo, na fursa ya kubadilishana mawazo kuhusu changamoto za kielimu kupitia mwangaza uliopo katika Neno la Mungu.
Campus Night kwa kawaida hufanyika mwanzoni mwa au katikati ya mwezi Oktoba kila mwaka.  Sababu ya kuwa na Campus Night katika majira hayo ni ili kwamba pawepo na ushiriki mkubwa wa wanafunzi kwa kuwa katika majira hayo vyuo na shule ndio zinakuwa tu zimefunguliwa.
Walengwa ni wanafunzi katika Chuo cha Ualimu Songea, Chuo cha SAUT, St Joseph University,  Open University-Ruvuma Region, Chuo cha Waganga Wasaidizi- MATC, pamoja na Shule za Msingi na za secondari zote  zilizopo katika manispaa ya Songea.
Ndani ya SRC idara hii imegawanyika katika makundi matatu;  nayo ni:-

MUDA WA KUKUTANA:
1.     CA’s Wajumbe wa Injili wa SRC – Ahamisi Saa 10:00 – 12:00 jioni.
2.     CA’s Vijana Chipukizi wa SRC – Kila J’mosi Saa 03:00 – 05:00 Asub.
3.     CA’s Huduma Ya Mashuleni: Mashuleni & Vyuoni - KILA IJUMAA MCHANA

Idara Ya Wanafunzi Na Watoto
Ya Kanisa La SRC.
Watoto ni Mbegu Njema kwa ajili ya kanisa la kesho. Idara hii ya watoto ni moyo wa kanisa la SRC, tukiamini kwamba mtoto akilelewa katika njia impasayo kuiendea hataiacha kamwe hata atakapokuwa mzee.
Ni malengo na mtazamo wetu kwa watoto kwamba idara ya watoto inawagawanya watoto katika makundi mawili. Kundi la kwanza ni la umri kati ya miaka 5-13, Kundi la pili ni lile lenye umri kati ya miaka 13-17.
Kazi za idara hii inajumuisha kupanga mipango ya kwenda kuhudumu mashuleni pamoja na kutengeneza masomo ya Neno la Mungu kwa ajili ya kwenda kufundishia katika mashuleni na vyuoni.

1 comment: